Image

ZANZIBAR ELECTRICITY CORPORATION
(ZECO)

Image
MSAJILI WA HAZINA, WAJUMBE WA BODI YA ZECO , MENEJIMENT YA ZECO PAMOAJA NA WATENDAJI WA OFISI YA MSAJILI WA HAZINA ZANZIBAR

MSAJILI WA HAZINA, WAJUMBE WA BODI YA ZECO , MENEJIMENTI YA ZECO PAMOAJA NA WATENDAJI WA OFISI YA MSAJILI WA HAZINA ZANZIBAR

Msajili wa Hazina, Wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi ya ZECO, Menejimenti ya ZECO pamoja na watendaji wa Ofisi ya Msajili wa Hazina Zanzibar wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kumaliza mafunzo ya Sheria ya Ofisi ya Msajili wa Hazina Zanzibar yaliyofanyika Ofisi za ZECO Gulioni tarehe 28/09/2024.

 

USAMBAZAJI UMEME MAENEO YA KILIMO KANGAGANI PEMBA

USAMBAZAJI UMEME MAENEO YA KILIMO KANGAGANI PEMBA

Waziri wa Mji, Nishati na Madini Mheshimiwa Shaibu Hassan Kaduara ametembelea na kukagua maendeleo ya mradi wa usambazaji umeme katika mashamba ya kilimo Kangagani kisiwani Pemba.

Kufika kwa huduma ya umeme katika mashamba hayo, yataongeza fursa za ajira kwa wakaazi wa maeneo hayo na kukuza kipato cha mtu mmoja mmjoa na Nchi kwa ujumla. 

UFUNGAJI WA VIFAA VYA KUSAWAZISHA UMEME (VOLTAGE REGULATOR)

UFUNGAJI WA VIFAA VYA KUSAWAZISHA UMEME (VOLTAGE REGULATOR)

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maji, Nishati na Madini Ndg. Joseph Kilangi akiongozana na watendaji wa Wizara hiyo pamoja na watendaji wa Shirika la Umeme Zanzibar (ZECO) wakiwa katika ziara ya kutembelea mradi wa ufungaji wa vifaa vya kusawazisha umeme mdogo unaotekelezwa na Kampuni ya NOVAVIS INTERNATIONAL katika eneo la Kitogani Wilaya ya Kusini Mkoa wa Kusini Unguja.

Ufungaji wa vifaa hivyo unatarajiwa kukamilika ikifikapo mwishoni mwa mwezi wa Novemba, 2024 ingawa itaanza kufanya majaribio ifikapo mwishoni mwa mwezi wa Oktoba, 2024 na inatarajiwa kupunguza tatizo la umeme mdogo kwa asilimia 95.

Jumla ya maeneo nane (8) yanatarajiwa kufungwa kwa vifaa hivyo kama vile; Tunguu, Kitogani kwa upande wa Kusini na Mahonda, Upenja, Donge, Fukuchani kwa upande wa Kaskazini na Chuini pamoja na Ubago kwa maeneo ya Kati. 

Cable Maintenance

Tumbatu Island Cable Maintanance

ZECO, technicians are working on the construction of an underground cable from Mkokotoni to Tumbani after the cable suffered a rupture.

The importance of this   service will open investment opportunities for the island of Tumbatu.

ZIARA YA KUKAGUA MIUNDO MBINU NA VITUO VYA KUPOZEA UMEME

ZIARA YA KUKAGUA MIUNDO MBINU NA VITUO VYA KUPOZEA UMEME

Meneja Mkuu wa Shirika la Umeme Zanzibar (ZECO) Ndg. Haji Haji akisikiliza maelezo kutoka kwa Meneja Idara ya Huduma za ufundi na uzalishaji umeme Mhandisi Moh'd Zuber juu ya namna ufanyaji kazi wa kituo cha kupozea na kusambazia umeme kiliopo Mpendae Zanzibar.

Ziara hiyo imempa uwelewa Meneja Mkuu kujua changamoto mbali mbali zinazoikabili miundo mbinu ya umeme hapa Zanzibar.

USAMBAZAJI UMEME MASHAMBA YA KILIMO UMBUJI

USAMBAZAJI UMEME MASHAMBA YA KILIMO UMBUJI

Mafundi wa Shirika la Umeme Zanzibar (ZECO) wakiwa katika kazi ya usambazaji umeme katika mashamba ya kilimo katika kijiji cha Umbuji kinachopatikana Wilaya ya Kati Mkoa wa Kusini Unguja.

Kazi hiyo ya usambazaji umeme itawanufaisha wakulima hao kwa kuweza kufanya kazi zao za kilimo cha umwagiliaji maji kwa siku zote za mwaka.

Aidha, huduma ya umeme itaweza kufungua fursa za ajira kwa wakaazi wa maeneo hayo. 

UKAGUZI WA MIUNDO MBINU ILIYOIBIWA VYUMA

UKAGUZI WA MIUNDO MBINU ILIYOIBIWA VYUMA

Waziri wa Wizara ya Maji, Nishati na Madini Mheshimiwa Shaib Hassani Kaduara, Mkurugenzi Idara ya Nishati na Meneja Mkuu wa Shirika la Umeme Zanzibar pamoja na watendaji wa Wizara wamefanya ziara ya kukagua njia kuu ya kusafirishia umeme wa msongo wa 132 kilovolti ambapo watu wasiojulika wameiba vyuma vya miundo mbinu hiyo.  

MKUTANO WA MHESHIMIWA WAZIRI NA WAFANYAKAZI WA ZECO

MKUTANO WA MHESHIMIWA WAZIRI NA WAFANYAKAZI WA ZECO

Waziri wa Wizara ya Maji, Nishati na Madini Mheshimiwa Shaib Hassan Kaduara (ambae hayupo pichani) akizungumza na wafanyakazi wa Shirika la Umeme Zanzibar (ZECO) wakati wa mkutano wa kila mwaka wa kuzungumza na wafanyakazi hao.

USAMBAZAJI HUDUMA YA UMEME MASHAMBA YA KILIMO DONGWE

USAMBAZAJI HUDUMA YA UMEME MASHAMBA YA KILIMO DONGWE

Naibu Waziri wa Wizara ya Maji, Nishati na Madini Mheshimiwa Shaaban Ali Othman amezindua huduma ya umeme kwa wakulima wa Dongwe Wilaya ya Kusini Mkoa wa Kusini Unguja.