Image

ZANZIBAR ELECTRICITY CORPORATION
(ZECO)

Image
UFUNGAJI WA VIFAA VYA KUSAWAZISHA UMEME (VOLTAGE REGULATOR)

UFUNGAJI WA VIFAA VYA KUSAWAZISHA UMEME (VOLTAGE REGULATOR)

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maji, Nishati na Madini Ndg. Joseph Kilangi akiongozana na watendaji wa Wizara hiyo pamoja na watendaji wa Shirika la Umeme Zanzibar (ZECO) wakiwa katika ziara ya kutembelea mradi wa ufungaji wa vifaa vya kusawazisha umeme mdogo unaotekelezwa na Kampuni ya NOVAVIS INTERNATIONAL katika eneo la Kitogani Wilaya ya Kusini Mkoa wa Kusini Unguja.

Ufungaji wa vifaa hivyo unatarajiwa kukamilika ikifikapo mwishoni mwa mwezi wa Novemba, 2024 ingawa itaanza kufanya majaribio ifikapo mwishoni mwa mwezi wa Oktoba, 2024 na inatarajiwa kupunguza tatizo la umeme mdogo kwa asilimia 95.

Jumla ya maeneo nane (8) yanatarajiwa kufungwa kwa vifaa hivyo kama vile; Tunguu, Kitogani kwa upande wa Kusini na Mahonda, Upenja, Donge, Fukuchani kwa upande wa Kaskazini na Chuini pamoja na Ubago kwa maeneo ya Kati.