Image

ZANZIBAR ELECTRICITY CORPORATION
(ZECO)

Image
USAMBAZAJI UMEME MASHAMBA YA KILIMO UMBUJI

USAMBAZAJI UMEME MASHAMBA YA KILIMO UMBUJI

Mafundi wa Shirika la Umeme Zanzibar (ZECO) wakiwa katika kazi ya usambazaji umeme katika mashamba ya kilimo katika kijiji cha Umbuji kinachopatikana Wilaya ya Kati Mkoa wa Kusini Unguja.

Kazi hiyo ya usambazaji umeme itawanufaisha wakulima hao kwa kuweza kufanya kazi zao za kilimo cha umwagiliaji maji kwa siku zote za mwaka.

Aidha, huduma ya umeme itaweza kufungua fursa za ajira kwa wakaazi wa maeneo hayo.