ZECO YATAKIWA KUBORESHA HUDUMA
Shirika la Umeme Zanzibar (ZECO) limeshauriwa kuboresha huduma zake zaidi katika eneo la huduma za dharura ili kupunguza malalamiko kwa wateja wake.
Wakichangia ripoti iliyowasilishwa na Meneja Mkuu Shirika la Umeme Zanzibar juu ya utendaji wa Shirika hilo kwa mwezi Julai hadi Disemba 2020, wajumbe wa kamati ya Mawasiliano, Ardhi na Nishati ya Baraza la Wawakilishi katika afisi za Shirika zilizopo Gulioni Zanzibar wamesema kuwa licha ya Shirika kupiga hatua kubwa za usambazaji umeme pamoja na uimarishaji wa miundo mbinu ya umeme mapungufu yaliyobakia kwa Shirika ni kuchelewa kutatua matatizo kwa uharaka.
Wamesema kuwa kuboreka kwa huduma za umeme nchini kutapelekea kukuza uchumi wa nchi na hata kuongeza mapato ya Shirika jambo ambalo litapelekea Shirika hilo kuongeza gawio Serikalini.